Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.



Kosta magoroso.
Mashabiki na Wadau wengi wasoka hapa nchini licha ya kupitia katika nyakati tofauti ngumu katika soka la Tanzania Toka enzi za Jk Nyerere kamwe kuna baadhi ya wanandinga ambao walipata kutikisa soka la hapa nchini awawezi kuwasahau ,miongoni mwao ni Kosta Magoroso ambaye alicheza katika kiwango cha juu sana akiwa na Waziri Mkuu Dodoma,Tukuyu Stars Pamoja na Lipuli Ya Iringa.
Magoroso ambaye ni mzaliwa wa Iringa mjini Eneo la Mkwawa alianza kusakata kandanda katika shule tofauti za msingi kutokana na baba yake kuhama hama kikazi ambapo ilisoma katika mikoa ya Shinyanga ,mbeya ,morogoro,na Iringa katika shule ya Mlangari na baadae nyota yake iling’ara zaidi akiwa katika masomo ya sekondari.
Magoroso anaeleza  baada ya kumaliza masomo ya sekondari alianza kucheza soka la nguvu akiwa na timu ya vijana ya iringa mwaka 1986 timu ambayo iliundwa na wachezaji vijana ambao walisheheni vipaji vya hali ya juu na walifanikiwa kupata majina makubwa na kutingipsha soka la hapa nchini wakiwa na timu tofauti za ligi kuu.
Baadhi ya wachezaji hao ni Stivin musa [marehemu],Goerge Kumbemba,Dankani Buti Nini akiwa na reli ya Marogoro ,charamanda saidi [kurugenzi ya Dodoma],pamoja na Daud Kufakunoga [prisons ya mbeya.wengine ni Jems Mwagama Maji Maji ya Songea,Yusuph Kobe SDA Dodoma pamoja na Rajabu Juma  Ambaye aliweka na reli ya morogoro.
Baada ya kuchezea vijana ya Iringa kwa mafanikio makubwa  mwaka 1987 alisajiliwa na timu ya Waziri Mkuu ya Dodoma ali ambayo ilipelea nyota yake kuzidi kupea zaidi na  kuchaguliwa katika timu ya Taifa ya vijana kwa kuwa kipaji chake kionekana kwa kila aliyemwona uwanjani.
Mechi yake ya kwanza  katika michuano ya kimataifa walicheza na timu ya Taifa ya Sheli sheli mchezo ambao ulimalizika kwa sale ya bao 1-1 yeye akiiswazishia Tanzania katika dakika ya 90, pia mchezo wa pili walicheza na timu ya vijana Ya sheli sheli mchezo ambao kwa mara nyingine uliisha kwa sare ya bao 1-1 na  bao la Tanzania lilifungwa na Athumani China mara baada ya kupokea Pasi safi toka kwake na kukwamisha mpira kimiani,ambapo timu hiyo ilienda nchini Usheri sheri Mara baada ya kuarikwa katika sherehe  ya kitaifa ambayo ilifanyika nchini humo.
Baada ya kucheza timu ya vijana kwa mafanikio mwaka 1989 alibahatika kuitwa katika timu ya taifa ya Tanzania hali ambayo ilimfanya apagawe na kujisikia kama yupo peponi kwa kuwa habari za kujiunga na timu ya taifa kwa mara ya kwa aliambiwa na kaka yake na baadae akasikia kupitia Magazeti,yeye binafsi aliwanza sana kuhusu kuchaguliwa kwake na alijifikikilia jinsi ambavyo angecheza na wachezaji wakubwa ambao ailikuwa akiwasikia kwenye vyombo vya habari,na mara baada ya kujiunpga na timu alifanikiwa kuwafunika wachezaji wakonge ikiwemo kumnyang’anya namba Selestine Skinde.
Vile Vile mwaka 1989 alijiunga na Tukuyu Stars timu ambayo aliitumikia hadi mwaka 1992 na akatimukia timu ya nyumbani ya Lipuli Fc timu mbayo hakudumu sana na baadae akaitwa na timu yake ya zamani ya Waziri mkuu Dodoma timu na aliichezea adi mwaka 1996 ambapo kutokana na kuwa na mapenzi na timu yake ya nyumbani ya Iringa akaamua kurupdi Lipuli na akacheza hadi mwaka 2000 hapo ndipo akatundi Darga.
Mechi za kimataifa.
“nakumbuka mechi yangu ya kwanza nikiwa na timu ya Taifa ya wakuwa niliogopa sana kuingia ukwanjani kwa kuwa  mimi nilikuwa ni miongoni mwa wachezaji ambao walikuwa na umri mdogo katika kikosi chetu  ambacho kilichuana na timu ya daraja la kwanza toka Urusi mchezo ambao kocha alinipanga na nilifanikiwa kucheza vizuri hali ambayo ilipelekea nimnyang’anye namba Selestine Mbunga Skinde.
“ambapo katika mchezo ule ambao timu ya taifa ya Tanzania ilishinda bao 4-3 nilifanikiwa kufunga bao 2 kwa mikwaju ya penalti  ambazo nilizipiga kwa presha kubwa  kwa kuwa wachezaji wakongwe waliogopa kupiga ili wasiaribu rekodi zao endapo wangekosa zile penalti,kikubwa mchezo ule ulinijengea uwezo wa kujiamini   na kujituma katika michezo ambayo ilikuja mbele yangu.
“mchezo mwingine ninaoukumbuka ni Kati yetu Stars na Tmu ya Taifa ya Zambia mwaka 1990 katika michuano ya SADCC, michuano ambayo Zambia walichukua ubingwa  kwa kuzibebesha kapu la magori timu zote ambazo zilikuwa zikishiriki katika michuano hiyo.
Nakumbuka Tanzania tulichezea kichapo cha bao 2-0, na Zambia ambayo ilikuwa ikiongozwa na mchezaji  mahili aliyekuwa akisakata kandanda nchini Uholanzi kwa sasa ni Rais wa shirikisho la soka nchini humo ,michuano ambayo timu yetu haikufanya vizuri.
Imani za kishirikina.
“Zilikuwepo,zipo na zitaendelea kuwepo  imani ambazo kwa muda mwingine zinawafanya wachopezaji wabweteke badala ya kufanya mazoezi kwa juhudi na maharifa,kunatukio moja lilitokea uongozi wa timu ambayo nilikuwa nikichezea [jina linaifadhiwa] waliandika majina ya timu pinzani na kuyapeleka kwa a mganga  ambapo mganga aliyachukua yale majina na akayaweka mdomoni mwa kondoo na Yule kondoo akafukiwa katikati ya uwanja ili kuwaroga wapinzani wetu.
“Kweli katika mchezo ule tukiwa katika uwanja wetu wa nyumbani tuliibuka na ushindi wa bao 3-0,vile vile mwaka 1994 kulikuwepo na mechi kati ya Lipuli na wekundu wa msimbazi Simba kitu ambacho kilitokea katikati ya mchezo nyuki walitanda uwanjani hali ambayo ilipelekea wachezaji wote na waamuzi kulala chini ya uwanja  hadi nyuki walipoondoka tukio lile mashabiki wa soka waliliusisha na imani za kishirikina kwa kuwa  wale nyuki waliondoka bila kumng’ata mtu yeyote.
Tofauti Kati ya soka la zamani na sasa.
“sisi wachezaji wa zamani tulikuwa tunajielewa  sisi tulikuwa na kila kitu ambacho mchezaji anatakiwa kuwa nacho akiwa uwanjani,tofauti na hivi sasa wachezaji wanapewa vitu ambavyo wanatakiwa kuwa navyo nje ya uwanja wakati uwanjani hawajui ,Tatizo la soka letu lanzima watu wote wanaohusika na mchezo huo wajtambue na kila mtu atekeleze majukumu yake ipasavyo kwa manufaa ya soka letu.
Hawezi Kusahau.
“Niliigharimu Tanzania katika michuano ya Challenge michuano ambayo ilikuwa ikifanyika nchini kenya kwa kukosa Penalti ambayo ilisasabisha sisi tupoteze mchezo ule kwa bao 2-1 bao la Tanzania liliwekwa kimiani na  Juma mgunda , baada ya kumalizika mchezo ule niliumia sana lakini makocha pamoja na wachzaji  wezangu walinipa moyo na kunieleza kuwa hata wachezaji wakongwa wanakosa penalti hivyo sio jambo la ajabu.
Goti lilimtoa Tukuyu Stars.
“Mwaka 1992 nikiwa na tukuyu Stars niliumia goti katka mchezo dhidi ya Simba mara baada ya kukumbana na Goerge Masatu eneo la 18 wakati naelekea kufunga  baada ya mchezo ule Baba  aliniita kuja kutibiwa Iringa nikaamua  kuachana na Tukuyu Stars na  na kurudi iringa na nuikapata matibabu kwa kipindi cha miezi 5,ambapo sikurudi tena  Tukuyu nikamua kujiunga na Lipuli ya ilinga timu ya nyumbani.
“Kikubwa  ambacho kilikuja kunikuta Mara baada ya kuumia goti nilipoteza nafsi ya kuchezea timu ya taifa ya Tanzania taifa strs kwa sisi kuitwa kwenye timu ya taifa ilikuwa ni fahari kubwa na heshima ya pekee sana.
Nyota  wa sasa Hapa nchini.
“Mrisho Ngasa  ni mchezaji wa pekee sana kwa kuwa bado anacheza katika kiwango cha juu  tukilinganisha na wachkezaji wengi wa sasa wanachuja baada ya muda mfupi.
Mashabiki wanawapa pombe wachezaji.
“kwa kiasi kikubwa soka la Tanzania linauwawa na mashabiki ingawa hawajitambui,kinachotokea  ukiwa unafanya vizuri mara kwa mara mashabiki wanakuchukua kwenda kukunyesha pombe baa kama starehe kwao kitu ambacho kinasbabisha wachezaji kushuka viwango vyao kwa kuwa kuna kipindi mcheaji unajikuta unapata ofa za kunywa pombe na kustarehe mfurulizo ali ambayo ni hatari sana hasa kwa wachezaj wetu wa sasa ambao wanapenda sana Starehe.
Ushauri kwa Tanzania /timu za Iringa.
“yanalalamikiwa mambo mengi sana lakini pia tunaitaji kuwa na makocha wenye taaluma ya mpira,Tff  watoe mafunzo ya  ukocha kwa mikoa yote ili kuwapata  makocha wengi wenye sifa  pia TFF waachane na tabia ya kutoa mafunzo kwa kuweka vituo katika mikoa michache ali ambayo inapelekea  washiriki kutumia gharama kubwa  na wengine kukata tama.
“Mkoani Iringa hatuna timu ya ligi kuu  tangu Lipuli iliposhuka daraja miaka 12 iliyopita hali ambayo ni haibu sana kwa mkoa wenye sifa kama Iringa kukosa timu ya ligi kuu ,tuwaunge mkono Kurugenzi pamoja na lipuli ili tuweze kuwa na timu ya ligi kuu misimu ijayo.
Baada ya kustafu soka.
“kwa sasa mimi ni mwakirishi wa Vilabu vya Iringa hapa nchini[TFF] pia ni kocha mwenye vyeti  lakini kubwa zaidi ni Katibu [IDYDC]Iringa Deveropment of youth Disabled and chidren care ambao wanatoa mchango mkubwa kwasoka la Iringa,kwa sasa nina miaka 43 nina mke na watoto 4,anahitimisha Magoroso ambaye alikataa ofa Toka Simba na Yanga zaidi ya Mara 4 kwa kuofia kuweka Rehani Maisha  chake.


Chapisha Maoni