Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.





Na Sophia Mwaipyana ,Mbeya

Maisha  ni safari ndefu ambayo binadamu tunasafiri huku hatujui safari hiyo inaishia wapi ikiwa  imeambatana na mipango mingi ambayo kila binadamu anatamani ifanikiwe ilikuweza kumwaongezea nguvu ya safari yake lakini kunawakati tunakutana na vikwazo vingi ambavyo vinaweza kufanya ukakata tama lakini tunaambiwa kukata tamaa nisawa na kujiroga mwenyewe.
Bahati Mwaipopo alikuwa na mipango mingi  aliyo tamani kutimiza  kupitia soka lakini alikutana na vikwazo vingi hali iliyo pelekea lengo lake la kupata kazi kupitia soka kugonga mwamba.
JELAMBA ilifanikiwa kufanya naee mahojiano kuhusu maisha yake ya soka ambapo aliatufahamisha kuwa  alianza kucheza soka toka akiwa darasa la tano katika shule ya msingi Mbalizi  hadi mwaka 1987 akiwa shule ya sekondari Kipoke  aliiwakirisha nyanda za juu kusini katika mashindano ya Umisenta taifa yaliyo fanyika mkoani Shinyanga  .
Timu yake ya  kwanza kuichezea ni timu ya Young Stars  ya Mbalizi mwaka 1989 -1991 na mwaka 1993 aliichezea timu ya  Benki kuu  na mwaka 1994 -1996 aliichezea timu ya Ujenzi Rukwa na mwaka 1997 aliichezea Tukuyu Stars  hadi mwaka 1998 alihamia katika timu ya 44kj iliyokuwa mbalizi ni timu ya jeshi.
Kwanini Tukuyu Stars hukudumu
“Kipindi kile mpira ulikuwa haulipi kama sasa kwahiyo lengo langu kubwa nilikuwa nataka nipate timu ya jeshi ili nipate kazi na ndiyo maana nikaenda katika timu ya jeshi lakini bahati mbaya zaidi sikuweza kutimiza ndoto yangu ya kuingia jeshini kupitia kipaji changu”


Mechi ngumu kwako
“Ni ile mechi ya mwaka 1995 Ujenzi na Yanga  mwaka huo Yanga ilikuwa inaitwa Yanga Kampara kwasababu walikuwa wametoka kuchukua ubingwa Uganda na mechi hiyo tulifungwa goli  nne  na mechi ilikuwa ngumu sana kwetu  kutokana na timu hiyo kusheheni wachezaji wazuri”
Tukio gani ambalo huwa halisahau
“nimatukio kama mawili hivi huwa siyasahau katika maisha yangu lakwanza ni ile ajari ya  basi mwaka 1992 nikiwa naichezea Benki kuu  tulikuwa tunaenda Tabora kucheza na  Polisi Tabora”
“Tulipofika kijiji kimoja kinaitwa Kasulu dereva alikuwa katika mwendo kasi gafla akaona mtu mbele sasa ile anataka kumkwepa  gari likahama njia ila namshukuru mungu wachezaji tulipata majeraha tuu hakuna aliye poteza kiungo wala maisha”
“chakushangaza hata tulipofika Tabora waligoma kutusogezea mechi kwahiyo tulicheza hivyo hivyo na tukatoka sale ya goli moja’
‘Pia mwaka 1996 nikiwa ujenzi  nakumbuka tulienda kucheza mechi na timu ya Waziri mkuu Dodoma tulikaa siku nne tukiwa tumeishiwa pesa yakula hadi pesa ya kuweka mafuta katika gari ili kurudi Rukwa’
“Kwahiyo wachezaji tukawa hatuna chakula wale wenye uwezo tulikuwa  ukimchukua mchezaji mmoja unaenda naye kula chakula cha mchana  jioni tena unaenda kula na  chezaji mwingine”
“Alitokea msamaria mmoja ambaye ni mkazi wa Sumbawanga akatupa pesa ya kujaza mafuta ambayo yatatufikisha Mbeya  kwahiyo tulipofika Mbeya mimi nikaisafirisha timu na nikaenda kurudishiwa pesa tulipo fika Sumbawanga”
Kwanini ujenzi ilipoteza mwelekeo
“Unajua mkuu wa mkoa kipindi kile timu inafanya vizuri mkuu wa mkoa alikuwa Chrisanti Mzindakaya kwahiyo alikuwa anaipa sapoti sana timu pamoja na Padri Msakira kwani ilikuwa hadi kambi tunaweka  misheni wakati mwingine chini ya usimamizi wa padri”
“kwahiyo shida ilikuja pale Mzindakaya alipo hamishwa na kuja mkuu wa mkoa mwingine ambaye alikuwa hapendi michezo kwahiyo shida ilianzia hapo timu ikayumba mishahara ikawa hakuna tena wachezaji tukaweka mgomo na wakatuambia asiye taka aondoke mimi na wenzangu kama watatu  tuliondoka”
Ushirikina katika soka
“Ushirikina upo sana  sema kuna utofauti kila timu ina utaratibu wake timu nyingine  wanafanya viongozi na nyingine hadi wachezaji mnashirikishwa ,mfano kuna wakati wachezaji tulikuwa tunaamshwa usiku tunaenda kuchezeshwa  mpira makaburini”
‘Nakumbuka   kunasiku tulikua tunacheza  Iringa  katika uwanja wa Samora sikuhiyo mimi nilikuwa ndiyo kapteni kwahiyo kabla ya mechi wakati wenzetu wanavaa mimi na golikipa tulitolewa na kupelekwa mto Lwaha ‘
“Tulipo fika kule nilipewa njiwa nimnyonge njiwa huyo alikuwa amefungwa sanda nyeusi nikamnyonga alafu nikaambiwa nimtupie katika mto huku nikinuwiza baada ya hapo tukaondoka kwenda uwanjani”
“Lakini chaajabu tulipo fika uwanjani   mechi ilikuwa ngumu sana  na tulifungwa goli 3-1 kwahiyo ushirikina katika soka upo sana  ila hauna faida yoyote zaidi ya kupoteza mwelekeo wa timu kwasababu  mkiamini sana  hiyo imani ndiyo pale mtapoteza mechi nyingi sana”
Kwanini ushindani kipindi hiki ni mdogo
“Timu zote iliifanye vizuri lazima   iwe na wadhamini kwahiyo tunaona kwasasa wadhamini wamebaki tu katika timu za dar-es-saalm na ndiyo timu hizo zinakuwa na ushindani mkubwa kwasababu wachezaji wanapata mahitaji yote kwa wakati’
“Kwahiyo hali hii inaziathili sana timu zetu za mikoani ukiangalia zamani timu nyingi zilikuwa zinawadhamini wake  ukiangalia Mecco ilikuwa chini ya shirika la ujenzi yani timu nyingi zilikuwa na wadhamini wao hasa mashirika binafsi”
“lakini sahizi tunaona mabadiriko kwa huyu mdhamini ambaye ameanza kuja hadi mikoani  kuwadhamini Mbeya City na Ndanda Fc kwahiyo wadhamini wajitokeze ilituweze kuongeza ushindani katika ligi yetu ‘
“Zamani timu nyingi zilikuwa zinachukuwa ubigwa kutokana na hilo lakini kwasasa tunabaki tu simba Yanga  unaona mfano safari hii mabigwa ni Azam kwanini sababu wanamdhamini wao ambaye ameifanya timu ilete mabadiriko katika ligi kuu”
Mafanikio
“Kama nilivyo kwambia zamani mpira ukipata mafanikio makubwa nikupata ajira siyo vinginevyo zaidi zaidi ni kutembea Nchi nzima na kufahamika”
 Mchezaji gani unaempenda hapa Tanzania
“Ni Canavaro Yule nimchezaji  sababu kiwango chake hakishuki na hana utani akiingia uwanjani hata kama nimechi ya kirafiki, pia ni mchezaji ambaye anacheza nafasi niliyokuwa nacheza mimi”
Wachezaji unao wakumbuka ulio cheza nao
“nikiwa ujenzi ni Atupele Mapungiro na nikiwa 44kj ni sajigwa jamaa alikuwa mvumilivu sana katika mazoezi na alikuwa na bidii”
Ushauri wako
“Mimi ushauri wangu ni kwa mashabiki wa Mbeya  tuzipe sapoti timu zote  ilizote ziweze fanya vizuri sasa tukiegamia upande mmoja je siku hiyo  timu tunayo itegemea isipo fanya vizuri itakuwaje, tukumbuke Prisons ndiyo timu toka zamani ilikuwa inatuwakirisha katika soka”
 
Familia
“nina familia ya watoto sita ila kati yao namuona mwanangu Girbet  ndiye atarithi kipaji changu kwani nyota njema huonekana asubuhi “
Maisha ya sasa
“Sahizi ni mjasiriamari napia naichezea timu ya maveterani ya Mbalizi na ninaishi huko  katika mji mdogo wa Mbalizi,na sitegemei kuacha kabisa kucheza soka kwasababu  napenda niupe mwili wangu mazoezi”


Chapisha Maoni