Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.






Mwandishi Alex Mapunda.
Isihaka Majaliwa Kabeya.
 UKIITAJA Maji Maji ya miaka ya 1983-1998 ambayo ilikuwa tishio kwa soka la Tanzania , bila shaka  lazima utamkumbuka Isihaka Majaliwa Kabena ambaye yumo katika orodha ya makipa ambao  walikuwa na uwezo mzuri wa kulinda lango hapa nchini.
Majaliwa ambaye ni mzaliwa wa Mihomboni , Iringa Mjini ni mtoto wa 12 kati ya watoto 14 kwa Mama Mmoja  alibahatika kuzaliwa mwaka ambao Tanganyika ilipata uhuru toka kwa mwingereza [1961] ambapo amezugumzia hisitoria yake ya
“Nilianza kucheza soka Darasa la Tano katika shule ya msingi Mwembetogwa Iringa Mjini,ambapo watu wengi walianza kukiona kipaji changu kutokana na umahili ambao nilionesha pindi nilipokuwa langoni.
“Baada ya kumaliza shule ya msingi,  mwaka 1976 nilijiunga na Afrikani Wanderers ya Iringa timu ambayo ilikuwa inashiriki mashindano ya mkoa huko ndiko nilianza kucheza soka la ushindani katika timu ambayo niliduma kwa misimu miwili,ila  1979 timu ya  reli ya Iringa ikanisajili na kufanikiwa kucheza kwa mafanikio makubwa.
“Kutokana na kujituma na uwezo niliounyesha mwaka 1983 nikatua Maji Maji ya Songea nikiwa hapo nyota yangu iling’aa zaidi na kiwango changu kuimalika zaidi kwa kuwa nikiwa na timu hiyo tulifanikiwa kuchukua ubingwa  hapa wa kombe la muungano mara mbili mfurulizo ,na baada ya kucheza na wanalizombe kwa muda mrefu hatimaje mwaka 1989 nikarudi nyumbani Iringa kutumikia Timu Ya Mazao ya shirika la usagishaji  Tanzania hata hinyo mwaka 1991 nikaachana na mambo ya soka na kujikita na kilimo ambacho naendelea nacho adi leo.
Hakucheza  Simba,Yanga.
“Toka nilipoanza kucheza soka sikuwa na ndoto za kuchezea timu za  Simba na yanga kwa kuwa kipindi hicho Timu ya Maji Maji ilikuwa kubwa na ilikuwa inaudumia wachezaji kuliko Timu zingine hapa nchini .
Llakini pia kuna ushauri niliupata toka kwa Sadi Ali ambaye aliwai chezea Timu ya Simba pindi nilipokuwa  Afrikani Wanderers, kuwa nisijiunge na timu hizo hata kama nikipata nafasi ila hakuniambia kwa nini,lakini hata hivyo sikupata nafasi za kuzichezea Timu hizo.
Stasahau
Mwaka 1983 kulikuwepo na mechi kali sana kati yetu na Simba toka jijini Dar es salam mechi hile ilichezwa wakati kamati ya ufundi ya Simba ilikuwa inaongozwa na kikosi ambacho kilikuwa kimesheni vichwa toka Brazil na wakati tunakutana nao Simba ilikuwa imezindua mfumo mpya wa kibrazili maarufu Kama ‘Kanivo Samba’ hakika simba ile ilikuwa inatisha.
“Lakini kilichotokea  uwezi kuhamini lakini itabidi uhamini kwa kuwa ndivyo ilivyotokea,na nikiwa kama mlinda mlango Namba 1 wa timu  yetu Viongozi wakanichukua na kunipeleka kwa  Mganga wa jadi ambaye sasa ni Marehemu ili kuchukua mbinu za kuidhibiti Simba.
“Wakati wa asuhuhi  nakumbuka mganga aliniambia kuwa, mechi itakuwa ngumu sana kutokana na uimala wa wapinzani wetu,usiku wa leo nimejitaidi kuokoa magoli mengi sana kadili ya uwezo wangu lakini hata hivyo yamebakia magoli mawili ambayo nitayamalizia uwanjani wakati mechi ikiendelea.
“Wakati wa mchezo ulipowadia timu zote zikaingia uwanjani na mechi ikaanza,mechi ilikuwa ngumu sana na Simba walipata bao 2 za wazi lakini waamzi wa mchezo ule wakayakataa na kusema wafungaji waliotea[off side] na hadi mwisho wa mchezo  tukatoshana nguvu ya bila kufungana.
“Hapo ndipo nilipokumbuka maneno ya mganga,kwa kweli siwezi kusahau ni tukio ambalo lilinitokea moja kwa moja nikiwa na timu ya Maji Maji.
Mechi  ninayokumbuka
“Mechi kati ya Mji Maji  ya Songea  na CDA Dodoma mechi ambayo tuliibuka na ushindi wa bao 1-0 bao ambalo ligubikwa na utata mkubwa hadi ikasababisha mechi kusimama kwa takribani dakika 14,na mwamzi wa pambano lile Mzee Dastan Daffa na mwamzi wa Pembeni Amed yasni kutoka Mpwapwa  wakuamru mpira uende kati kati wakimaanisha ni goli.
“Lakini ukweli wenyewe mpira ambao ulipigwa na Madaraka Suleiman toka winga ya kulia ulitoboa wavu wa pembeni kwa nje na kutumbukia ndani ambapo waamuzi walipoona wavu unatikisika na mpira upo ndani wakajua moja kwa moja ni goli na hadi mwisho wa mchezo maji maji moja CDA sifuri.
Mechi ya kimataifa
“Ulikuwa ni mchezo wa kimataifa kati yetu na Mofulila Wanderers toka mchini Zambia hatua ya makundi michuano ya Afrika mashariki,katika mechi hiyo jopo la waamzi wakiwemo mmjo toka Malawi  na mmoja toka Zazibar waliufuata uongozi wa maji maji wakiitaji Takrima kwa ajili ya kuipa msaada timu yetu wakati wa mchezo lakini,kutokana na aliyekuwa kiongozi wa yanga   Isa Makongoro kufungiwa Maisha kwa kosa la Rushwa uongozi wa Maji Maji ukakataa kutoa chochote kwa msaada wa timu yetu.
“Tukio lile lilifanya jopo la waamzi lilikasirika sana na wakahaidi kuifanyia ukatili maji maji wakati wa mchezo na ndivyo ilivyotokea  ambapo mchezo ulikuwa mgumu sana kwa maji maji na kila timu yetu ilichokifanya kilionekana kibaya huku faulo zikiwa nyingi na muda wote washabuliaji wa maji maji walikuwa wakiunasa mpira basi ni [off side na hadi mwisho wa mchezo Tulifungwa Bao 2-1 na kutupwa nje.
Makocha wa kigeni na Wazawa
“Tatizo la hapa nchini makocha wazawa wanapuuzwa tofauti na makocha wa kigeni ambao wanapewa kila kitu wanachoitaji ,kama makocha wenyeji wangewezeshwa kama wa kigeni soka letu lingekuwa na ushindani toka kwenye ngazi za chini.
“Tff na vilabu vyetu lazima zizingatie hilo mimi sioni kitu cha ajabu ambacho wanakifundisha makocha wa kigeni ambacho wazawa wamekikosa.
Ushauri kwa Watanzania
“Lazima lazima tuwe wavumilivu  tusipende kupanda na kuvuna wakati huo huo, lazima tuwe wavumilivu kwa kujenga soka letu huku Tukijikita Zaidi kwa Soka la Vijana,na kuepuka Siasa katika soka.
Wachezaji  wanaomkosha.
“mimi binafsi namkubari sana kiungo wa yanga Frenk Domayo ambaye amefanikiwa kumwamisha namba Haruna  Niyozima mchezaji wa kimataifa toka nchini Rwanda pia Mtanzania anayekiputa soka la kulipwa nchini Kongo mbwna Samatta ni wanacheza Vizuri.
Baada ya Soka.
“ Toka mwaka 1991 nilianza kazi ya kilimo ambayo hadi hii leo  inanifanya mimi na familia yangu kuendesha maisha yetu ya kila siku lakini Soka zaidi ya kufahamika na kujuana na watu sikufaidika na lolote zaidi kupata posho ambayo haikututosheza kwa wachezaji wa kipindi kile ikilinganishwa na wachezaji wa sasa”,Huyo ndiye majariwa ambaye amekili wazi kuwa wakati akicheza alikuwa akinyanyaswa  na Zamoyoni Mogera.
mwisho


Chapisha Maoni