Ads (728x90)

Inaendeshwa na Blogger.






Na Alex Mapunda[mwandishi]
Stivin Mapunda 
 
Garrincha wapili toka kushoto waliochuchumaa
Stivini mapunda [Garrincha] ni miongoni mwa washambuliji hatari sana ambao wamewai tokea hapa nchini na akafanikiwa kutikisa soka la Tanzania kuanzia mwaka 1997-2005.akichezea timu ya  Maji Maji ya Songea ,Wekundu wa Msimbazi ‘Simba’ na Timu ya Taifa [99-2005]
Garrincha alianza kucheza soka toka shule ya msingi Hanga, Darasa la tatu akiwa na miaka 9 na akiwa sekondari alifanikiwa kushiriki michuano mbali mbali ya shule pamoja na Umiseta hadi ngazi ya Taifa ambapo kipaji chake kikaonekana na kuanza kung’ara nchi zima.
katika kipindi hicho akiwa shule ya msingi Garricha alipata nafasi ya kwenda kucheza soka Ulaya kupitia kwa mzungu aliyekuwa kocha wa maji maji wakati huo ambaye alikiona kipaji chake wakati timu hiyo  ilikuwa ikiweka kambi mara kwa mara huko Hanga, lakini baba yake alikataa kutokana na kuofia usalama wa mwanao kwa kuwa  alitaka mwanao asiende mbali nae.
“Kocha wa maji maji kipindi hicho toka Toka barani Ulaya alitaka kunichukua ili nikasome ulaya Pamoja na kuendeleza kipaji changu cha Soka baada ya kukiona kipaji changu shuleni Hanga wakati wao walipokuwa wameweka kambi, bahati mbaya baba yangu alikataa kwa kuofia usalama wangu pindi nitakapo kuwa mbali nae hivyo ikashindikana.anasimulia mapunda.

mwaka 1993 Mapunda alianza kucheza soka la ushindani akiwa na timu ya Taiger mbeya timu ambayo alicheza kwa kujituma sana ambapo kiwango chake kiliongezeka siku hadi siku na mwaka 1997 alitua rasmi katika Timu ya Maji maji maarufu kama wanalizombe toka mkoani Ruvuma.
mapunda alicheza kwa umaili mkubwa akiwa na maji maji ambapo aliiwezesha timu hiyo kuchukua ubingwa wa Tanzania kwa mara ya Tatu mwaka 1998 katka ligi ya muungano na yeye alifunga magori ambayo yaliiwezesha timu yao kuchukua kombe la ligi ya muungano kwa mara ya tatu.
Garrincha aliwataja baadhi ya wachezaji wa kikosi cha wanalizombea ambao  walichukua ubingwa mwaka 1998 ni pamoja na Ivo Mang’itu[marehemu],John Alex,Amri Said,Wile Martin,Stivin Mapunda,Twaa omari[marehemu],Godfrey kikumbizi,Kelvin haule,Said msham[marehemu] pamoja na Omari Husein ambao waliipeleka Maji Maji kwenye michuano ya kimataifa.
Hata hivyo kutokana nyota yake kuendelea kung’ara kwa kiwango cha hali ya juu sana na kusakwa na timu kubwa hapa  nchini  ilimlazimu kuipa kisogo timu yake ya nyumbani na akajiunga na Wekundu wa msimbazi Simba,mwaka 1999,timu ambayo aliichezea kwa mafanikio makubwa sana na aliisaidia timu hiyo kunyakua mataji mbali mbali iiwemo kombe la Tasker,ligi kuu bara, pamoja na kombe la mapinduzi lakini kubwa zaidi alisaidia kuifikisha Simba kwenye robo fainali ya clabu bingwa afrika mara baada ya kuwasambalatisha vigogo wa soka toka  Misri[ Zamareck] kwa mikwaju ya Penalti na kufanikiwa kuingia Robo Fainali.
Safari yao katika ligi ya mabingwa iliishia Robo fainali mara baada ya kuchezea kipigo toka kwa Mabingwa wa Ivory [Isec Mimosas] katika mechi ya marudiano ambayo Simba walichezea Ugenini na hatimaye wakaaga Rasmi mashindano.
Kurudi Maji Maji.
“mwaka 2005 niliamua kurudi maji maji kutokana na migogoro ambayo ilikuwepo ndani ya clabu ya Simba hali ambayo ilipelekea mimi na mwezangu kufungiwa pasipo kujua kosa letu na kututaka kuandika barua kwa kuwa sikuwai gombana na mtu yeyote ndani ya Simba nikaamua kuondoka kwa Moyo mweupe na kurudi  katika timu yangu ya Zamani Maji Maji sc.
“niliendeleza soka nikiwa na maji maji  toka milipo Toka Simba kwa misimu Kadhaa na baadae nikaamua kutundika daruga na kujishughulisha na shuguli za kawaida.
Tukio ambalo sitasahau.
“mwaka 2004 tulifungiwa chumbani siku 4 nchini Nigeria na ubarozi wa Tanzania ili kutunusulu tusikamatwe mara baada ya kuchelewa toka nchini Benin ambako tulitoka kucheza kati yetu na timu ya Taifa  ya Benin mechi ambayo tulifungwa goli 4-0,na mara baada ya kufika Nigeri tulikosa usafiri mara baada ya kukuta ndege ambayo tulitakiwa kusafiri nayo  imeongoka na kipindi hicho Tayari visa yetu ya kubaki nchini humo ilikuwa imekwisha.
“Barozi wa Tanzania inchi Nigeria SiSiko ilimlazimu kutufungia chumabani huku tukila nyama kipande kimoja na mkate mara moja kwa siku kama Gerezani kwa uzembe ambao ilifanywa na viongiozi wetu,na hatimaye siku ya 4 tulifanikiwa kuondoka na viongozi wetu hawakuwai kuzungumzia chochote kuhusu tukio lile.
“Inanisikitisha sana kwa timu ya taifa kukwama ugenini kwa kipindi cha siku 4, mimi binafsi kwa kipindi chote cha maisha yangu hapa duniani siwezi kusahau”.alisema mapunda.
Ugomvi na ndolanga
“Sababu za mimi kugombana na mwenyekiti wa Fat Mhidin Ndolanga zilisababishwa na kocha wa timu ya Taifa kipindi hicho ambaye pia alikuwa kocha wa timu ya prisons ya mbeya Charles Boniface mkwasa kuwapanga wachezaji wa timu yake ya Prisons katika mechi ngumu nchini Rwanda kati yetu na Rwanga kwa kuwapa uzoefu wachezaji wake ili wafanye vizuri ligi kuu bara,na kuwaacha wachezaji muhimu nikiwemo mimi, ambao tulikuwa tunaaminika ni wachezaji wazuri.
“Wakati mechi ikiendelea Ndolanga alimtuma mjumbe wake kuja kumhuliza kocha kwa nini mapunda hajaaza katika kikosi cha kwanza?,kocha alikaa kimya baadae akajibu ataingia,wakati huo hata wachezaji wezangu benjini walimwambia mapunda inatakiwa aingie akaokoe timu kwa kuwa tayari tulikuwa tumeshafungwa goli 1 hata hivyo kocha hakuchukua maamzi yeyote.
“Lakini zikiwa zimebaki dakika tano mpira kumalizika Mkwasa akaniita kwa Hasira nikapashe ili niingie nikaamua kukataa kwa kuwa muda ulikuwa umeisha hali hiyo ilimkasilisha  na akaamua kuandika ripoti ya jumla kuhusu mechi hile kuwa Mapunda alikataa kucheza tangu mwanzoni mwa mchezo ali ambayo ilimfanya mwenyekiti wa Fat akasilike na kusema kuwa Sitacheza timu ya Taifa hadi hatakapo ng’atuka madarakani.
“Ugomvi wetu ulikuwa mkubwa hadi ukasababisha waziri Juma kapuya kumfungia Ndolanga kutokana na vurugu ambazo zilifanyika mara kwa mara kwa wadau na mashabiki wakishinikiza nicheze  mpira,lakini mara baada ya Ndolanga kurudi Madarakani na kukaa kiti kimoja kuzungumzia mgogoro wetu na yeye kujua Tatizo, mambo yote yakaisha na hadi hivi sasa mimi na Ndolanga ni  Marafiki wa kudumu.
Mechi anayoikumbuka
“Naikumbuka sana mechi ya Clab bingwa kati yetu Simba na Timu ya jeshi toka Botswana,mwaka2003 ili kuwa mechi muhimu kwetu na tulicheza katika kipindi kigumu ambapo wachezaji 5 muhimu wa simba walikuwa wamefungiwa na mimi nilipewa jukumu la ukepteni na mechi hiyo ilichezwa uwanja wa Taifa  jijini Dar es salam,mechi ambayo tulipata ushindi dakika ya 89 ya mchezo goli ambalo liliwekwa kimiani na mimi mwenyewe bara baada ya kubanwa sana na ngome ya ulizi ya Timu hiyo.
“Watu wengi wakizani kwamba mechi ya marudiano Tutatolewa kutokana na ushindi mwembamba ambao tuliupata nyumbani lakini mambo yakawa tofauti, tukiwa ugenini tulicheza kwa morali kubwa na tukafanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 3-0,na tukafanikiwa kusonga mbele ambapo mechi iliyofuata tulipambana na Zamareck ya Misri.
Mchezaji ninayempenda
“Wachezaji wengi wanacheza vizuri lakini mtanzania anayekipiga Tp Mazembe nchini kongo Mwana Samatta, nampenda sana ni mchezaji ambaye anatambua cha kufanya pindi awapo uwanjani.
Beki msumbufu kwangu
“kiukweli mabeki walikuwa wananiogopa,mara nyingi nilikuwa nakabwa na mabeki wane,watatu, kwa kuwa nilikuwa mtu hatari sana ,mabeki wote nilikuwa nawaweza.
Ushauri wake kwa Timu ya Maji Maji.
“Viongozi wazieshimu pesa za club,na wahakikishe wanapigana hili kupata pesa za kuendeleza timu, wa ajili ya mafanikio ya wanamaji maji.
Kuyumba kwa Simba.
“Tatizo ni migogoro ilkiyopo ndani ya uongozi,simba sio timu mbovu,kinachotakiwa ni viongozi kuondoa tofauti zao ili kurudisha heshima ya Simba ambayo ni Timu kuwa hapa nchini.
“Lakini pia kupanga kikosi mara kwa mara,kikosi ambacho sisi tulifika nacho robo fainali kilikuwa na uzoefu wa miaka mingi na tulikuwa tunacheza kwa kuelewana sana tofauti na kikocha cha Simba ya Sasa.
Ushauri kwa wachezaji wa sasa.
“Kutokana na kwenda kwa wakati  wachezaji wa Tanzania wafanye mpango wa kuwa na mwanasheria ambaye atakuwa anawakilisha matatizo ya wachezaji kwa uongozi wa timu ili kuepuka matatizo yanayojitokeza kwa wachezaji na uongozi pindi wanapodai haki zao kwa kuambiwa kuwa hawana nidhamu hii itasaidia kuwalinda wachezaji.
“asilimia kuwa wachezaji wanakosa uhuru kwa viongozi wa club na inafikia kipindi mchezaji akidai haki zake anafungiwa na kuambiwa amekosa nidhamu kutokana na viongozi wetu kujifanya wanajua kuliko wachezaji.
Maisha Baada ya Soka
“Hivi sasa nimeoa na nina mke na watoto 3 na umri wangu ni miaka 36 [adi kufikia 2013],namshukuru mwenyezi mungu kutonana na soka nafahamiana na watu wengi ambao wengi wao tunasaidiana katika maisha kiukweli mpira umenifungulia dira ya mafanikio yangu.
“Nina ofisi na najishugulisha na ukandarasi wa majengo pamoja na bara bara,lakini nafikiria kuwa na ofisi kubwa ili kuhakikisha najijenga vizuri zaidi kimaisha.
Zawadi kwa Watanzania.
“Nina mpango wa kujenga shule ya soka ‘sports academy centre’ambayo itafundisha mpira kuanzia ngazi ya chini ili kuwapata wachezaji wenye uwezo wa hali ya juu ya kucheza soka hapa nchini.
“Natarajia baada ya muda mfupi ujenzi utaaza kwa kuwa tayari taratibu za awali zimeshakamili na shule hiyo natarajia kujenga mkoani Ruvuma.alisema Garrincha.


Chapisha Maoni